b Kum 15:21; 12:5-6, 11; Mwa 8:20; Law 6:25; 17:9; 22:19-20, 27; Ezr 8:35; Mal 1:8; Kut 12:5; Ebr 9:14; 1Pet 1:19; Hes 6:16; Isa 58:5
c Kut 29:10, 15, 36; Law 4:29; 6:25; Eze 45:15; Mwa 32:20, 30; 2Nya 29:23-24; Kut 29:26; 32:30; Isa 56:7; Rum 12:1; Hes 15:25; Flp 4:18; Ebr 10:11
Leviticus 1:2-7
2 a“Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Yeyote miongoni mwenu aletapo sadaka ya mnyama kwa Bwana, alete mnyama kama sadaka yake kutoka kundi lake la ng’ombe au la kondoo na mbuzi. 3 b“ ‘Kama sadaka hiyo ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la ng’ombe, atamtoa ng’ombe dume asiye na dosari. Ni lazima amlete kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili aweze kukubalika kwa Bwana. 4 cAtaweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya kuteketezwa, nayo itakubaliwa kwa niaba yake ili kufanya upatanisho kwa ajili yake. 5 dAtamchinja yule fahali mchanga mbele za Bwana, kisha wana wa Haruni kuhani wataleta damu na kuinyunyiza pande zote za madhabahu yaliyo penye ingilio la Hema la Kukutania. 6 eAtaichuna hiyo sadaka ya kuteketezwa na kuikata vipande vipande. 7 fWana wa Haruni kuhani wataweka moto juu ya madhabahu na kupanga kuni juu ya huo moto.
Copyright information for
SwhKC